20 February 2015

Kijana anayesema ni mtoto wa Jay Z na kuhusu kesi yake dhidi ya rapa huyu.

jay-z-son-one
Rapa anayechipukia Rymir Satterthwaite anasema Jay z ni baba yake mzazi na anataka vipimo vya DNA. Kijana huyu mwenye miaka 21 anasema Jay Z alikuwa na mahusioano na mama yake kwenye miaka ya tisini na kwamba walikuwa pamoja kwa muda mrefu kabla hajawa maarufu.
 jay-z-love
Rymir anataka vipimo vya DNA Ila Jay z hajakubali kufanya hivyo ndio maana mpaka sasa kijana huyu amechukua hatua ya kwenda mahakamani kutaka mahakama ilazimesha vipimo hivyo.
Rymir analalamika kuwa ameishi kwenye maisha ya shida huku baba yake akiwa tajiri kwa muda mrefu. Jay Z anajulikana kuwa na mtoto mmoja tu ambaye ni Blue Ivy Carter na mke wake ambaye ni Beyoncé Knowles

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname