Msanii
akishafanikiwa kuwashawishi mashabiki kulipa kiingilio na kuingia
kwenye show yake, hana kazi ya ziada zaidi ya kufanya show nzuri ambayo
huwafanya mashabiki wenyewe kuingia tena mifukoni na kuwatunza kwa
misimbazi ya kutosha.Lady Jaydee kupitia Instagram ametuonesha noti za
msimbazi ambazo alitunzwa jukwaani na mashabiki waliohudhuria show yake
ya jana pale MOG.
Kwenye picha hiyo ameandika:
“Asanteni wote mlionitunza jukwaani Nilitoka kwetu na alfu 6 Nikarudi mkoba umejaa
Kazi
ya muziki nzuri jamani Ila Haka ka mkoba jana @niitesonga alikuwa
anataka kuka kwapua Mi mwenyewe nna madeni kibao Nawaza nianze lipi
kulilipa “
No comments:
Post a Comment