26 January 2015

MKAZI WA KINONDONI AWA MMLIKI MPYA WA UCHUMI SUPERMARKETS TANZANIA












UCHUMI SUPERMARKETS LTD TANZANIA
RE: MKAZI WA KINONDONI AWA MMLIKI MPYA WA UCHUMI SUPERMARKETS TANZANIA
Maduka makubwa yanayoongoza Tanzania ya “Uchumi supermarks” leo yameendesha droo ya mwisho ya kampeni yao ijulikanayo kama  “Mimi Mwanahisa promosheni” iliyofanyika katika tawi lake jipya la  Mbezi-Kawe.
Hafla hiyo ilishuhudiwa na Mheshimiwa Said Meck Sadik- Mkuu wa mkoa Dar es salaam ambaye pia alikua mgeni rasmi, Mheshimiwa Ezekiel Wenje-Mbunge wa jimbo la Nyamagana pamoja na mkurugenzi mtendaji wa Uchumi Afrika mashariki Bw. Jonathan Ciano

Bi. Elizabeth Robert ambaye ni mkazi wa manispaa ya kinondoni, Dar es Salaam aliyefanya manunuzi yake tarehe 22/12/2014 katika duka kubwa la Uchumi tawi la Shekilango ndie aliyeibuka mshindi wa  hisa za Uchumi supermarket zenye thamani ya Tsh 5,000,000/= baada ya kushiriki mara kwa mara katika promosheni hiyo iliyodumu miezi 3.

Mapema baada ya kuwaalika wageni mbalimbali wakiwemo waandishi wa habari katika hafla hiyo, ambapo pia ndio ilikuwa siku ya kuzindua rasmi tawi la Mbezi-Kawe lililopo maeneo ya mbezi chini karibu na klabu ya kijamii ya rainbow, mkurugenzi wa Uchumi supermarket Tanzania  Bw. Chris Lenana alisema “Kupitia shughuli zetu za kila siku, matawi yetu 5 sasa yanalipa kodi ya serikali kiasi cha millioni 600 kwa mwaka  tofauti na mwanzo milioni 50 kwa mwaka tulipokuwa na tawi moja tu”.

Bw. Lenana aliendelea kusema kuwa hadi hivi sasa Uchumi ina wafanyakazi 430 na imekua mstari wa mbele kabisa katika kukuza ajira kwa vijana sambamba na kuboresha mishahara ya wafanyakazi wake kila mwaka. Uchumi pia imekua ikiwajibika kusaidia jamii ambapo kwa kushirikiana na Amref wameweza kuchangia afya ya mama na mtoto. Hii ilidhihirika kwenye kampeni ya Simama kwa ajili ya akina mama wa Tanzania ilioanzishwa na AMREF kwa ushirikiano na Uchumi supermarkets.

Mkurugenzi mkuu wa maduka yote makubwa ya Uchumi Afrika mashariki Bw. Jonathan Ciano ambaye nae alipata nafasi ya kuzungumza alisifu maendeleo ya ukuaji mzuri wa maduka hayo makubwa na kusisitiza kuwa ulipaji ushuru ni kujitegemea akisihi makampuni mengine yaige mfano huo.

Kwa upande mwingine  Mheshimiwa Said Meck Sadik ambaye ndiye alikua mgeni rasmi wa hafla hiyo, alishukuru kwa kukaribishwa ili kuweza kuzindua duka hilo kubwa na kusifu ubora wa huduma na bidhaa za Uchumi na kuwahasa kuendelea hivyo hivyo.

“Bado sijaridhika na matawi matano tu, ninamatumaini makubwa kuwa mnaweza kwenda zaidi ya hapo” alisema Mheshimiwa Sadik. Aliyataja baadhi ya maeneo ambayo yana wingi wa watu kama Kibaha, Mbagala na Kigamboni akitolea mfano kuwa hayo ni maeneo wanayoweza kuwekeza ili watanzania waendelee kufaidika na huduma zao. Alitaja baadhi ya miji kama Mbeya, Mwanza na Arusha ambapo pia kuna fursa nzuri za biashara na wingi wa watu. “Dhumuni lenu liwe ni kuifikia angalau asilimia 60 ya watanzania wote hapa nchini na kutokana na hilo hata uchumi wa nchi hii utapata afya”…alimalizia Mheshimiwa.
Aliendelea kuwahasa watanzania wanaopewa nafasi kazi katika makampuni kama haya ya kigeni kuwa waaminifu, kuchapa kazi kwa bidii  na kuacha uzembe unaojitokeza kila mara na kisha kubaki kulalamika tu.
Ni takribani miaka minne sasa tangu Uchumi ianze kufanya biashara hapa nchini. Kampuni hiyo imekuwa na utaratibu wa kuwazawadia wateja wake kila mwisho wa mwaka na kwa mwaka huu Uchumi wameenda mbele zaidi kwa kutaka kuwafanya wateja wawe wamiliki halali wa kampuni hiyo tofauti na mwanzo ambapo zawadi zilizotolewa kama ni kama seti ya fanicha, Jiko Bab Kubwa na talii na uchumi.

 Kipindi hiki waliamua kuanzisha Mimi mwanahisa promosheni ambapo lengo la promosheni ni kumpata mshindi ambae angekuwa mmiliki wa Uchumi kupitia hisa (amana) zenye gharama ya Tsh. Milioni 5.

Promosheni hii ilianza rasmi tarehe 25 No 2014 na ilitakiwa kuifikia kikomo tarehe 15 Januari 2015 ambapo kipindi chote hiki mteja alitakiwa kufanya manunuzi ya bidhaa zenye jumla ya Tsh 20,000 na hapo basi angeingizwa kwenye droo ili kujaribu bahati yake nasibu ya kushinda zawadi mbalimbali zilizoorodheshwa na Uchumi hapo awali. Sambamba na zawadi ya hisa kwa mshindi mkuu, zawadi nyingine zilizoshuhudiwa zikitolewa ni kama ifuatavyo:- T.V bapa ya LG (Flat screen), Microwave, Water dispenser, Simu ya mkononi aina ya Techno H3, Ofa ya kufuliwa nguo kwa mwaka mzima, Chakula cha jioni kwa wapendanao watatu katika hoteli ya Serena Hotel ada za shule kwa watoto zenye thamani ya Tshs 600,000/=, vocha za manunuzi zenye thamani ya shilingi Tshs 720,000/= zitakazo tumika nchi nzima kwa kipindi cha mwaka mmoja.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname