15 November 2014

TAHADHARI MUHIMU KWA WANAWAKE


Baadhi ya watafiti wana sahuku ikiwa vipimo vya sketi vitamtahadharisha mwanamke kuhusu tisho la Saratani 
Utafiti unaonyesha kuwa wanawake wanaonenepa maishani bila ya kuwa waangalifu wanajiweka katika hatari ya kupata Saratani. 
Watafiti kutoka chuo Kikuu cha London wanasema kwamba wanawake walio kati ya umri wa miaka 24-28 ambao huendelea kunenepa kila baada ya miaka 10, wako katika hatari zaidi ya kupata Saratani ya Matiti baada ya kupitisha umri wa kuzaa. 
Sasa je ni nini ishara ya mwanamke kunenepa? Watafiti wanasema vipimo vya sketi yake vinaweza kukusaidia kujua ikiwa uko katika hatari ya kpatwa Saratni ya Matiti au la.
Kila unapogundua kuwa sketi yako inaendelea kuwa ndogo kiunoni, basi inakubidi ujue kuwa mwili wako unaongekeza kwa unene. Na pia ni rahisi kwa wanawake kukumbuka kipimo cha sketi kuliko kitu kingine chochote.
Kwa hilo watafaiti wanasema mwanampe anapaswa kutahadhari kila sketi yake inapoendelea kuwa ndogo kwake maana kwamba amenenepa zaidi. Ikiwa ukubwa wake unazidi kwa kipimo cha sketi mbili katika kipindi kimoja basi mwanamke anakuwa katika hatari ya kupatwa na Saratani hata zaidi. 
'Mfumo wa maisha'.SOMA ZAIDI>>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname