25 August 2014

HATIMAYE MTOTO MZURI LINAH AFUNGUKA KUHUSU BBA. NDOA YA AMINI NA MUZIKI!

Mwimbaji wa kike aliyepiga hatua kubwa hivi karibuni na kusainiwa na kampuni ya kubwa ya Afrika Kusini NFZ, Linah alifanya mahojiano exclusively na tovuti ya Times Fm na kufunguka zaidi kuhusu mambo muhimu katika muziki wake.Linah alizungumzia masuala muhimu yanayohusu muziki wake. Jinsi alivyofanya kazi na kundi la Uhuru ‘Ole Themba’ na alivyojipanga kulikabili soko la kimataifa.

Mwimbaji huyo alieleza pia mtazamo wake kwa ushirikiano kati ya wasanii wa kike na sababu inayowafanya kutokuwa pamoja na kusapotiana pamoja na mambo mengine.

Ameeleza pia kama ana mpango wa kwenda Big Brother na mtu anaempendekeza zaidi kwenda katika jumba hilo, na kuweka wazi reaction yake baada ya kupata taarifa kuwa aliyewahi kuwa mpenzi wake Amini amefunga ndoa kimyakimya.Isikilize hapa utapata taarifa kiundani kuhusu yote anayoyazungumza.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname