Miongoni mwa stori za town nilizozipata ni hii ya Mamba kuuwawa Block
41 Kinondoni Dar es salaam kwenye area ambayo wanaishi watu kadhaa
maarufu wa Tanzania akiwemo Kalapina wa kikosi cha Mizinga, hii ni nyuma
ya bestbite Mamba huyu akiwa ametokea kwenye bwawa nyuma ya 41
Records.
Bwawa limezungukwa na nyumba kwenye eneo la kwa Kisamo zamani Kajima
ambapo kwenye hili bwawa zamani kidogo kulikua na mamba wawili ila baada
ya kugundulika mmoja akachukuliwa na watu wa Wanyama ila mwingine
hakuonekana.
Tukio la jana ilikua saa nane usiku ambapo mamba huyu alijitokeza
barabarani mtaani ndipo majirani wakamuita mtu pekee mwenye bunduki
kwenye huo mtaa ili amuue kwa sababu mwanzoni kabla hawajajua walikua
wanahofia kumuua wakidhani ni kosa la kisheria.
Baada
ya kuuawa Defender ya Polisi ikamchukua huyo Mamba baadae alfajiri
ambapo unaambiwa kwenye picha hapa anaonekana mdogo ila ni Mamba mkubwa
kabisa, siku ya mvua aliwahi kutoka nje ya Bwawa tena ambalo alitisha
sana watu ila muda mfupi baadae akarudi ndani ya Bwawa
Ripota wa nguvu Ramaman kutoka Block 41 amenitumia hizi picha na
kusema walifanikiwa kumuua huyu Mamba baada ya kumpiga risasi nne
credit-millard ayo
No comments:
Post a Comment