04 May 2014

BREAKIN NEWZZZ:- MAPADRI 2 WAFARIKI GHAFLA KWENYE MAPOKEZI YA ASKOFU SOMA HAPA HABARI KAMILI LIVE!!

 Askofu Gervas Nyaisonga wa jimbo la Katoliki la Mpanda akisalimiana na Mapadri wa jimbo hilo katika eneo la mto koga Hapo jana ambapo ndipo linapoanzia Jimbo katoliki la Mpanda wakati alipokuwa akiwasili rasmi kwenye jimbo lake jipya la Mpanda akiwa anatokea jimbo la Dodoma 
 Askari  wa skauti wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda wakiwa katika eneo la daraja la mto koga wakimpokea askofu Gervas Nyaisonga alipowasili hapo jana akitokea jimbo la Dodoma ambapo askofu Nyaisonga alipokuwa analiongoza kabla ya kuhamishiwa Jimbo la Mpanda na amesimikwa jana kuwa askofu wa Jimbo la Mpanda

 Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo katoliki la Mpanda akibusu Ardhi hapo jana katika kijiji cha Kamsisi ikiwa ni ishara ya kuhamia rasmi kuliongoza jimbo la Mpanda akitokea jimbo katoliki la Dodoma


 Msafara wa waendesha pikipiki wakiwa katika eneo la uwanja wa ndege mjini Mpanda wakiwa wanaongoza msafara wa kumpokea askofu Gervas Nyaisonga hapo jana ambae amehamishiwa jimbo la Mpanda akitokea jimbo la dodoma
 Mapadri wa kanisa katoliki wakiwa kwenye kanisa kuu la jimbo Katoliki la Mpanda kabla ya kuanza kwa ibada ya kukabidhiwa ufunguo wa kanisa hilo askofu Gervas Nyaisonga ambae amehamishiwa jimbo la Mpanda ikiwa ni ishara ya kuyaongoza makanisa na kuyasimamia makanisa yote ya jimbo katoliki la Mpanda 

Picha na Walter Nguluchuma 
Katavi yetu Blog
******************
Na  Walter Mguluchuma

Padri  wa Kanisa Katoliki wa Jimbo la Mpanda Padri Matini Kapufi (42 ) pamoja na Katekista wa Kanisa hilo  wa KijiJI  cha  mtakuja  Parokia ya Inyonga  Katekista Patricki Mwendo  wa Saa (60) wamefariki   Dunia  baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka  baada ya gari kuacha  njia na watu wengine wawili kujeruhiw na kulazwa hospitalini

Kwa mujibu wa Kamanda wa jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri  Kidavashari ajari hiyo ilitokea hapo juzi  majira ya saa  nne asubuhi  katika Kijiji  cha Kamsisi   tarafa ya Inyonga barabara  ya  Inyonga  kuelekea Mkoani Tabora

Alisema ajari  hiyo ililihusisha gari aina ya  Toyota  Hilux pick Up  lenye  namba za usajiri  T 302 CUY lililokuwa likiendeshwa na  Marehemu Padri Martini Kapufi  ambae ni Paroko wa parokia ya Mwese  jimbo katoliki la Mpanda

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname