PUB
iliyoibuka kwa muda mchache na kukamata ‘taito’ kubwa Bongo ya
mwigizaji Aunt Ezekiel, Demonte imefungwa ghafla, haitoi huduma
tena.Imedaiwa kuwa, pub hiyo iliyopo maeneo ya Mwananyamala, jijini Dar,
imefungwa kutokana na mhusika kushindwa kuiendesha.
“Imefungwa, nasikia gharama za vinywaji na wafanyakazi aliowaajiri
zilikuwa juu akaona bora afunge,” alisema rafiki wa Aunt aliyeomba
hifadhi ya jina lake.
Paparazi wetu alishuhudia pub hiyo ikiwa imefungwa kwa zaidi ya miezi
kadhaa, alipomtafuta Aunt, hakupatikana hadi tunakwenda mitamboni.
No comments:
Post a Comment