Nzumari
za Mombasa, Eve ‘Queen’ Adhiambo amelazimika kuziahirisha tuzo za mwaka
huu katika dakika za mwisho kutokana na mahudhurio hafifu na maandalizi
ya zimamoto.
Eve
Hadi
saa nne usiku, sound system na jukwaa vilikuwa havijawekwa na watu
wachache waliokuwa wamehudhuria walilazimika kurudi makwao baada ya
kuzuiwa kuingia ndani ya ukumbi sababu mambo yalikuwa hayajakaa sawa.
Eve ambaye alionekana kupagawa wazi alisema kuwa watu waliokuwa wameenda
walidanganya na watu wachache getini kwamba show hiyo ilikuwa
imeahirishwa.
“Unajua
kulikuwa na watu kwenye geti waliokuwa wakiwahadaa watu waliokuwa
wamekuja kwa kuwaambia kuwa tukio lilikuwa limeahirishwa, hizi ni tetesi
kubwa na nahisi iliwafikia hata wale waliokuwa wamepanga kuja,” Eve
aliiambia website ya ommydallah.com.
“Ntalazimika sasa kusitisha tukio hili mpaka ntakapotangaza tena kwakuwa bado nahitaji kuwatuza washindi,” aliongeza.
Eve
aliwalaumu pia wafundi wa sauti aliowapa kazi kuishughulikia na kusema
kuwa walichelewa kwenda.Hata hivyo mmoja wa mafundi hao aliiambia tovuti
ya . Ommydallah kuwa ni Eve ndiye alichelewa kuwataarifu.
“Huyu
demu sisi mwanzo alitufuata jana (Friday) akitaka sound then sasa leo
ndio akaja vizuri tena saa tisa na sisi mdosi akatutuma kazi na
tukaja, lakini nadhani shida ilikuwa ni mambo na pesa maana watu wengi
hapa wanaogopa kufanya kazi na huyu dem,” alisema.
Eve
alikanusha madai hayo na kusema kuwa kilichotokea ni hujuma. “Unajua
sipendi kumtukuza shetani na nikisema kuwa kuna mkono wa mtu nitakuwa
namtukuza ila ningependa kusema kuwa usishangilie wakati mwenzako
amepatakina na shida kama hii maana kesho inaweza kuwa wewe,” alisema.
Rapper Nay wa Mitego aliyekuwa ameenda Mombasa kuhudhuria show hiyo
alilazimika kulipia mwenyewe gharama za malazi na tiketi ya ndege
kurejea Dar kwakuwa mwandaaji hakuweza kuingiza fedha za kuweza kulipa
gharama hizo.
“Unajua
kaka me nimetoka Nairobi kushoot clip na nikaunganisha direct na hapa
but mambo ni kama unavyoyaona, cha msingi nilichokua nataka kutoka kwao
ni wanipe ticket yangu ya ndege tu ya kurudi bongo asubuhi maana
nina show na Diamond kesho,” ameiambia tovuti hiyo. “Kama bahati mimi
hutembea na hela zangu mfukoni maana nayajua mambo haya sasa itabidi
nijilipie tu kila kitu na hela yangu.”
Hata hivyo Nay aliyekuwa ametajwa kuwania tuzo hizo amesema amemsamehe Eve.
“Yani
kulingana na heshima na ukubwa wangu unadhania mimi nastahili
kuhangaika hivi?!! inakera sana ila huyu dada mimi nishamsamehea.”
Drama
nyingine iliyotokea ni baada ya Eve na timu yake kuamua kuondoka
ukumbini ambapo watu waliokuwa wamelipa kiingilio walimfuata kudai
warudishiwe chao. Watu hao walirushiana maneno na timu ya Eve japo
hawakuambulia chochote.
Rich Mavoko alikuwa ahudhurie show hiyo pia lakini machale yalimcheza.
Pamoja
na Nay Wa Mitego wasanii wengine waliokuwa wametajwa kuwania tuzo hizo
ni pamoja na Ommy Dimpoz, Lady JayDee na Rich Mavoko
No comments:
Post a Comment