Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’.
Sosi wa karibu na mwigizaji huyo, amenyetisha habari kuwa, mwanaume
huyo (jina kapuni) aliyedaiwa kuwa ndiye mwenye ujauzito huo ambaye
maskani yake ni Kinondoni, jijini Dar, alimshushia kipigo Aunty Lulu kwa
sababu ya kumuonea wivu kwani amekuwa akimzuia hata kuongea na simu.
Sosi huyo alizidi kutiririka na sentensi kuwa, kutokana na kipigo
hicho, Aunty Lulu aliumia na kuanza kuvuja damu kisha akakimbizwa
hospitali kwa Dokta Mvungi (Kinondoni) ambapo aliambiwa mimba
imeharibika na kulazimika kusafishwa kizazi.
“Vikao vya kumsema mwanaume huyo kwa kosa alilofanya vilifanyika
nyumbani kwao Jumapili ambapo aliahidi kutorudia tena na kuomba radhi
huku akiahidi kumfanyia makubwa Lulu,” alisema sosi huyo makini.
Baada ya paparazi wetu kuzinyaka habari hizo, alimwendea hewani Aunty
Lulu, alijibu kwa unyonge na kusema ndoto zake za kuwa na mtoto
zimeyeyuka kufuatia kipigo hicho.
“Sina la kusema zaidi, ndoto za kuwa na mtoto zimeyeyuka mwanaume
huyu amezidi wivu lakini sina jinsi kwa sababu ndio baba mtoto na
ameshaomba msamaha,” alisema Lulu.
-gpl
No comments:
Post a Comment