23 December 2013

Ishara za Yondani zazua utata Simba

BEKI wa kati wa Yanga, Kelvin Yondani ‘Vidic’, ameibua maswali mengi kwa mashabiki wa Simba na Yanga baada ya kuvua jezi yake namba tano na kuwatupia mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi ambao nao waliichanachana na kugawana vipande.
Lakini kabla ya kutupa jezi hiyo, aliwaonyeshea ishara ya pesa kwa kuchezesha mikono yake ndipo utata ulipozidi. Yondani aliibua maswali hayo ni baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu na mwamuzi wa mchezo huo, Ramadhani Ibada ‘Kibo’, kutokana na kumwonyesha kadi ya njano kwa mara ya pili.
Alipokuwa anatoka nje, ndipo Yondani alipofanya tukio hilo kwa kuwarushia mashabiki wa Simba jezi ya Yanga. Mashabiki wale waliichukua na baada ya muda mchache, waliichanachana vipande vidogo.
Mmoja wa mashabiki wa Simba, Hassan Timbwa, alisema: “Hakuna jinsi, ilikuwa lazima tuichane kwa sababu kwetu hakuna mvaaji, sisi Simba rangi zetu ni nyekundu na nyeupe, si nyingine.”
Yondani hakuwa wazi kufunguka juu ya mkasa huo na kuondoka kimya kimya. Katika mechi hiyo ya Nani Mtani Jembe, Simba ilishinda mabao 3-1.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname