06 November 2013

SUMAYE AAMUA KUMVAA LOWASSA HADHARANI...SOMA ZAIDI HAPA

Dar es Salaam.Vita ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 imeingia katika sura mpya baada ya Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye kumlalamikia mrithi wake katika wadhifa huo, Edward Lowassa akimtuhumu kumfanyia mbinu chafu.

Huku akinukuu habari iliyoandikwa na gazeti hili Septemba 16, 2013 yenye kichwa cha habari, ‘Lowassa afichua siri ya mradi wa maji Ziwa Victoria’, Sumaye alisema Lowassa amekuwa akimfanyia propaganda na mbinu chafu.


 


Katika habari hiyo, ambayo Lowassa alialikwa katika Harambee ya kuchangia Shule ya Msingi ya Kanisa la AICT huko Kahama, Shinyanga hivi karibuni, alikaririwa akisema mawaziri watatu, tu ndiyo waliounga mkono wakati alipopendekeza kutekelezwa kwa mradi huo kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri cha Serikali ya Awamu ya Tatu iliyokuwa chini ya Benjamin Mkapa.


Lowassa, ambaye katika kipindi hicho alikuwa Waziri wa Maji na Maendeleo ya Mifugo, aliwataja mawaziri waliounga mkono mradi huo kuwa ni Rais Jakaya Kikwete ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Mohamed Seif Khatibu, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais.


Akizungumza na waandishi wa habari jana, Sumaye


Alisema hizo ni mbinu chafu zilizokuwa na lengo la kumpaka matope… “Najua mhusika ametumia sana mradi huu kisiasa na sisi wengine tumenyamaza japo ukweli tunaujua. Amenilazimisha niseme ukweli kuhusu mradi huu kwa sababu mimi nilikuwa Waziri Mkuu na mradi umetekelezwa chini ya uangalizi wangu,” alisema na kuongeza:


“Kama Waziri anaweza kubuni na kutekeleza mradi mkubwa hivyo peke yake, akiwa Waziri Mkuu si maji yangefika Dodoma? Mbona hata bado kuna kuna sehemu za Kanda ya Ziwa bado kuna shida ya maji?” alihoji Sumaye, ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika Serikali ya Awamu ya Tatu.


Alipotafutwa kwa simu kuelezea madai hayo, Lowassa, ambaye yuko Dodoma akihudhuria vikao vya Bunge, alisema hawezi kubishana na Sumaye kwa kuwa anamheshimu kwani amewahi kuwa kiongozi mkubwa serikalini.


“No comment’ (sina la kusema), siwezi kubishana na Sumaye kwani amewahi kushika nyadhifa za juu katika nchi hii,” alisema Lowassa, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli (CCM).


Sumaye alimtuhumu Lowassa kwa kusema uongo na kuongeza kuwa amefanya kosa la jinai kutoa siri za Baraza la Mawaziri.


“Pamoja na kwamba hilo lililoelezwa ni uongo mkavu, mhusika kama waziri mwandamizi wakati huo na sasa anawinda nafasi kubwa katika nchi, hakutegemewa kutoa siri za Baraza la Mawaziri, labda amediriki kufanya hivyo kwa sababu anajua anayosema siyo ya kweli, vinginevyo ni kosa la jinai na akishtakiwa anafungwa jela,” alisema.


Sumaye alisema hizo ni mbinu chafu zinazofanywa dhidi yake kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.


“Ziko mbinu nzuri na za kistaarabu na ziko mbinu chafu kama za kupakana matope (character assassinations). Mtu wa kwanza anajisafishia njia yake kwa kufyeka miiba na kuondoa magogo njiani ili wakati ukiwadia, mbio zake zisikwazwe na vigingi vyovyote. Aina ya pili ya mbinu chafu ni pale mhusika anapotengeneza mbinu za kuwamaliza wengine wanaodhaniwa kuwa washindani wake,” alisema Sumaye.


Hata hivyo, alipoulizwa kama amejipanga kugombea urais mwaka 2015, Sumaye alisita kujibu kwa muda mrefu, lakini baadaye akajibu:


“Nasema hivi, kama ni kugombea nina haki zote, kama ni uwezo ninao, kama ni imani ya Watanzania kwa sehemu kubwa ninayo. Kilichobaki ni uamuzi tu wa mimi kutamka. Kwa hiyo sijatamka msije mkasema nagombea urais. Nasema tu na mimi katika Watanzania wanaofikiriwa na mimi nasikia nimo. Kwani ninyi hamnifikirii? Sasa itakapofika huko mbele, si tutaamua wakati huo?”

-Mwananchi

1 comment:

  1. Upon look at you actually give up so that you can dining with the girlfriend plus fake audemars piguet to the weeknights – upon look at this converse with high regard nonetheless would not get in touch with outside, evaluate people plus all the things I'll manage to pay for. Convinced it might be expensive nonetheless it has the amount contains make sure to get client satisfaction. The values to get name brand different watches as well contains shopper favorable rolex replica sale just like gain plus return scheme to make certain that easier going with finding anything you totally desire plus have the choice to come back plus return it will this product failed to connect with a person's benchmarks. Cost ways will be safe and sound, bendable design a user's suitability. Shipping charges fake rolex for sale plus time-span either are certainly acceptable plus deviates while using site when supplement is required to be presented. Internet variety includes given a person mouse click admission to diverse country's plus foreign companies fake products and solutions by using just about very similar benefits plus panerai replica with primary merchandise. Several pertaining to name brand different watches is definitely that you may expect its excellence if hublot replica sale reaches resilience.

    ReplyDelete

Comments system

Disqus Shortname