12 November 2013

MWANADADA ''RACHEL HAULE'' AINGIA NA ''VANESSA'' (IN DILEMA) SOKONI... CHEKI HAPA



MWIGIZAJI wa kike katika tasnia ya filamu Swahiliwood Rachel Haule amesema kuwa sasa anasimama kama mtayarishaji na kutengeneza filamu zake mwenyewe na kwa kuanza kaanza na filamu yake ya kwanza ya Vanessa in Dilema ambayo ipo sokoni hivi karibuni huku akiamini kuwa ili upate maslahi ni lazima uwe mtayarishaji na muigizaji na ndicho alichokifanya.


Rachel akiwa katika pozi




Filamu ya Vanessa in Dilema

“Unajua hata mtoto anaanza kwa kutambaa kisha anakuja hatua nyingine ya kusonga mbele zaidi, hivyo hata mimi nimepitia hatua hizo na kujikuta sasa ni mtayarishaji wa filamu na ni mwigizaji kwa kufanya hivyo unaweza kupata maslahi na kuona faida ya filamu,”anasema Recho.

Msanii huyo anasema kuwa msanii aliyemtia moyo na kuchochea juhudi zake na kujikuta anakuwa ni moja kati ya mabinti wanaosimama na kuwa naye katika kundi la wanawake wachapakazi ambao ni watayarishaji ni Odama na Johari ambao ni tofauti na wasichana wengi wasiojituma na kutengeneza filamu zao, tofauti na kusubiri kucheza filamu tu.
CREDIT: FILAMUCENTRAL

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname