18 July 2013

NIPO TAYARI KUPIGANA NA JACK WOLPER ENDAPO ATAENDELEA KULITUMIA JINA LANGU KUJIPATIA UMAARUFU"...BABY MADAHA

Staa  wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph ‘Baby Madaha’ ameomba pambano la ngumi dhidi ya Jacqueline Wolper ili waweze kumaliza ubishi wa bifu lao.


Akipiongea na  mwandishi wetu, Baby alisema amechoshwa kusikia tambo za mpinzani wake huyo hivyo kama kweli ni mwanamke, wakutane kwa  ngumi  ili amuoneshe cha mtema kuni.


 “Asiniambie mimi natafuta kiki, mimi ni msomi kuliko yeye, arudi shule au akauze vipodozi. Najua kuimba, kuigiza na ni msomi yeye anaweza hayo? 


"Kimsingi naomba pambano nimtoe  manundu.Nipo  tayari  kupigana  naye  ili  nimshikishe  adabu,” alisema Baby Madaha. 

1 comment:

  1. msomi habwabwaj ujinga cjaona elmu yake imemsaidia nin we pga kelele tu wakat watu wanafanya yao unaeza mpga hzo ngumi zako lakin kiukwel Wolper kakupga gape la maendeleo mbal sana tafta maendeleo acha kutafta shari na watu walioendelea!!!

    ReplyDelete

Comments system

Disqus Shortname