11 April 2013

HUYU ndo Mwanaharakati maarufu wa mashoga Zambia aliyetiwa mbaroni.

 
Mwanaharakati maarufu wa haki za mashoga nchini Zambia Paul Kasonkomona amekamatwa na polisi baada ya kuonekana akifanya mahojiano katika kipindi cha ‘Live’ katika luninga
moja  nchini humo akihamasisha mahusiano ya jinsia moja  yahalalishwe.
Mkuu wa polisi Solomon Jere amekaririwa akisema Paul Kasonkomona ameshitakiwa kwa kuihamasisha jamii kushiriki katika katika matendo yasiyokubalika.
Alitiwa kizuizini wakati akitoka katika studio za televisheni hiyo inayomilikiwa na Muvi TV katika jiji hilo.
Vitendo vya mahusiano ya jinsia moja nchini humo ni kinyume cha sheria za Zambia.
Hata hivyo baadhi ya wananchi nchini humo wanachukulia hatua hiyo kama kinyume na haki zao.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname