03 January 2013

SAJUKI KUZIKWA IJUMAA MCHANA KISUTU.

Juma Kilowoko

Marehemu Sajuki enzi za uhai wake msanii huyu anatarajia kuzikwa Ijumaa.
MAZISHI ya msanii mahiri wa tasnia ya filamu Juma Issa Kilowoko ‘Sajuki’ anatarajia kuzikwa siku ya Ijumaa mchana katika makaburi ya Kisutu baada ya sala ya Ijumaa, akiongea na FC leo Rais wa shirikisho la Filamu Tanzania Simon Mwakifwamba amesema kuwa msiba huu unasimamiwa na shirikisho na wasanii wa filamu na wadau wa tasnia ya filamu.
Wasanii wa filamu Bongo

Baadhi ya wasanii wa filamu wakiwa msibani leo nyumbani kwa Sajuki Tabata Bima.
Zamaradi Mketema

Mtangazaji wa Clouds Tv Zamaradi akiwa na waombolezaji msibani kwa Sajuki.
Simon Mwakifwamba

Mwakifwamba Rais wa TAFF.
Juma Kilowoko

Sajuki akiwa katika picha enzi za uhai wake.
“Tumeamua kulichukua jukumu la kumzika msanii mwenzetu Sajuki na familia wabaki na shughuli nyingine kwa sababu amemwacha mke na motto ambao kwa vyovyote watahitaji kuishi kwa hiyo  kama kuna kidogo basi kiwasaidie, kwa hiyo tayari kuna kamati inayoshughulikia hilo,”anasema Mwakifwamba.
Rais wa TAFF alimedai kuwa bajeti ya awali kuanzia leo hadi siku ya mazishi gharama au fedha inayohitajika ni milioni Saba ambazo wadau mbalimbali na wasanii bado michango inahitajika hivyo Mwakifwamba anaomba wale wote wanaoguswa na msanii huyo hata kama si wasanii lakini wana michango yao wafike msibani na kuwakilisha michango hiyo.

Comments system

Disqus Shortname