09 February 2016

RAIS KABILA AWAZAWADIA MAGARI YA KIFAHARI WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA BAADA YA KUSHINDA MICHUANO YA CHAN..KILA GARI TSH. MIL 130

Wachezaji wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamezawadiwa magari ya kifahari baada ya kushinda Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani (CHAN).
Rais Joseph Kabila amemtunuku kila mchezaji gari gari la kifahari la thamani ya $60,000 (£40,000).
Wachezaji hao pia wamepewa nishani.


  • Wachezaji wa DR Congo walakiwa kishujaa
Chui hao wa Kinshasa walitwaa kombe kwa kulaza Mali 3-0 kwenye fainali na kuwa taifa la kwanza kushinda kombe hilo mara mbili
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2016/02/09/160209162219_dr_congo_chan_640x360_afp_nocredit.jpg

Mwandishi wa BBC Mbelechi Msochi anasema mchezaji Heritier Luvumbu Nzinga aliyeumia kwenye michuano hiyo pia ameahidiwa kwamba atasafirishwa ng'ambo kwa matibabu.
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2016/02/09/160209164033_dr_congo_players_kabila_512x288_bbc.jpg
  Rais Kabila amewapongeza wachezaji wa timu ya taifa

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname