16 October 2015

MASTAR MBALI MBALI NCHINI KU SUPPORT “AMANI KWANZA CAMPAIGN”





BARNABA BOY MSANII WA BONGO FLEVA


IRENE PAUL MSANII WA BONGO MOVIE  NA KAMAFA RADIO PRESENTER

YOUNG DEE

DOCTA D-ONE


MO MUSIC MSANII WA BONGO FLEVA




KABURU KIONGOZI WA SIMBA

Mastar mbalimbali wa hapa nchini wamejitokeza kwa moyo wote kushirikiana kwa karibu na shirika la  Global Peace Foundation Tanzania katika kuhamasisha Amani katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu ambao unatarajia kufanyika siku ya tarehe 25 October 2015.

Global Peace Foundation Tanzania ( GPFTZ)  ni  Tawi la Taasisi ya Kimataifa lisilo la Kiserikali na isiyotengeneza faida Global Peace Foundation (GPF) yenye makao makuu yake  Washington DC, nchini Marekani na  lenye matawi zaidi ya 16 duani,   .  Ni shirika linalo hamasisha kutetea na kulinda Amani dunia ,  shirika hili linaamini ya kuwa “ Kwa Mungu sisi wote ni familia moja”

GPF inafanya kazi kwa karibu na mitandao ya kiserikali na watu binafsi katika kuendeleza jamii, taifa na  kujenga na kulinda misingi na maadili katika jamii husika.

GPF ina rekodi nzuri ya kufanya kazi kwa karibu na kwa mafanikio makubwa  kuhamasisha na kulinda Amani katika nchi mbalimbali dunia katika bara la Afrika, Asia, Ulaya na Amerika.

Kwa upande wa Afrika, shirika hili limekuwa likijihusisha na maswala mbalimbali ya kijamii katika nchi za Kenya, Uganda na Nigeria kudumisha Amani kwenye ukanda wa Afrika.

Tarehe 31 August 2015 shilirika hili lilizindua Campaign yao iliyojulikana kama “AMANI KWANZA”  Kampeni hii imeandaliwa maalumu kwa malengo yafuatayo:

§  Kuwahamasisha Wanawake na Vijana kuwa mabalozi wazuri wa  kulinda na kuitetea Amani ya nchi yetu hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi
§  Kujiepusha na vitendo mbalimbali  ambavyo vinaweza kuchochea uharibifu wa Amani nchini
§  Kuhamasisha kila mmoja ashiriki uchaguzi kwa amani

Akizungumza na muandishi wetu, Ndugu Martha Nghambi, ambae ni Mkurugenzi mkazi wa shirika hili alisema campaign inaendelea vizuri, wamekuwa wakitumia social media zaidi kama vile kurasa za Faceboob, Twitter na Instagram ili kuhakikisha wana wafikia vijana wengi zaidi ambao ni zaidi ya 60% ya watanzania wote na pia ni kundi la muhimu sana katika kulinda amani.  Hali kadhalika Martha alisema wametoa wimbo maalumu wa kuhamasisha amani ambao umeimbwa na  mwana mziki maarufu Barnaba  Boy
“ bofya hapa chini kuuliza wimbo huo”

Kuungana na Global Peace Foundation Tanzania kuhamasisha Amani nchini tafadhali wa follow: Twitter: @globalpeacetz, Facebook: globalpeacefoundationtanzania na Instagram  globalpeacefoundationtanzania

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname