Staa
wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu. Gonjwa hilo limegundulika hivi
karibuni machoni mwa paparazi wetu baada ya kumuona mlimbwende huyo wa
Tanzania mwaka 2006 akiwa na bonge la nundu nyuma ya shingo, jambo
lililomfanya paparazi ashindwe kujizuia na kuamua kumuuliza Wema.
Habari
mbaya ikufikie kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Endless Fame Films
Productions ambaye yupo kwenye harakati za kuwania Ubunge wa Viti Maalum
kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Singida, Wema Isaac Sepetu
amegundulika kuwa na gonjwa la ajabu linalomsababishia kukosa raha
ambalo linakua kadiri siku zinavyosonga.
Bila
kupepesa macho Wema alisema kuwa ‘uvimbe’ huo upo mwilini mwake kwa
zaidi ya miaka 26 sasa na umekuwa ukiongezeka siku hadi siku.
Wema
alilazimika kufunguka zaidi baada ya paparazi wetu kumuona sehemu hiyo
ikiwa imemvimba bila kujua kama ni tatizo lake la miaka yote.
No comments:
Post a Comment