Kwa mujibu wa gazeti la The Telegraph,
mchejazji wa klabu ya Liverpool na timu ya Taifa ya Italia Mario
Balotelli jana amemiss mazoezi ya kwanza ndani ya klabu yake baada ya
kupata msiba wa Baba yake aliyewahi kumlea kipindi ana miaka mitatu.
Msiba huo uliotokea mwisho mwa wiki
iliyopita umemfanya Balotelli achelewe kufika mazoezini, ambapo sasa
ameongezewa likizo lakini uongozi wa klabu ya Liverpool unaamini
mchezaji huo atawahi kujiunga na wenzake siku yoyote kabla ya mwisho mwa
wiki ijayo ambapo Liverpool itasafiri Mashariki ya mbali na Australia
kwa ajili ya mechi za kujipima nguvu.
Baba huyo mlezi alikuwa anaitwa Francesco na amefariki huko nchini Italia
No comments:
Post a Comment