Wema Isaac Sepetu ‘Madam’
SALAMU
nyingi zikufikie mrembo usiyechuja umaarufu tangu mwaka 2006, Wema
Isaac Sepetu ‘Madam’ vipi uko poa? Mishemishe zinakwendaje?
Ukitaka
kujua afya yangu, mimi namshukuru Mungu kwani ni mzima, hofu na mashaka
ni kwako wewe uliye mbali na upeo wa macho yangu. Kitambo kidogo
kimepita sijakuona lakini naamini u-mzima wa afya.
Mbali na
kukusalimia, dhumuni la barua hii ni kutaka kukumbusha juu ya umuhimu wa
mdomo wako kuwa na staha. Kuna vitu vya kuzungumza lakini kuna ambavyo
vinapaswa kuwekwa ‘spea’.
Binafsi sikufurahishwa na namna ambavyo
ulimpa maneno makali aliyekuwa rafiki yako, Kajala Masanja kupitia
kipindi cha televisheni wiki iliyopita.Si busara kumtusi mwenzako
hadharani kiasi kile. Hata kama amekukosea kiasi gani, wewe ni mtu
maarufu unapaswa kuhakikisha kile unachokizungumza kitakuwa na matokeo
gani mbele ya jamii inayokuzunguka.
No comments:
Post a Comment