NEWZZ!!:- WATU 9 WAKAMATWA NA POLISI MOROGORO WAKIWA NA VIFAA VYA KIGAIDI
Watu 9 wamekamatwa wakiwa wamejifungia kwenye
msikiti wa Soni Morogoro wakiwa na vifaa vya milipuko hatari! Watu hao
ni watanzania"!!
Katika purukushani hizo polisi mmoja amenusurika kuuawa baada ya kukatwa na jambia shingoni.
================
By Standalone
Watu 10 wakamatwa msikitini wakiwa na milipuko, sare za jeshi, 'bendera ya Al Shabaab'
Watu 10 wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro baada ya kukamatwa
msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi
inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab wa nchini
Somalia.
Katika tukio hilo, mmoja anayesadikiwa kuhusiana na watu hao
waliokamatwa aliuawa na wananchi wenye hasira baada ya kumjeruhi kwa
panga askari polisi aliyekuwa akipambana naye.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa polisi mkoani Morogoro,
Leonald Paul alisema tukio hilo limetokea jana (Aprili 14 mwaka huu)
majira ya saa 3.30 usiku katika kitongoji cha Nyandero, tarafa ya Kidatu
wilayani Kilombero.
===updates===
Kamanda
huyo alitaja vitu vilivyokutwa katika mabegi yaliyokuwa ndani ya
msikiti huo ni pamoja na milipuko 30, bendera nyeusi yenye maandishi ya
Kiarabu yakisomeka ‘Mungu Mmoja’, majambia, bisibisi, vinyago vya
kuziba uso (masks), nguo za jeshi, misumeno ya chuma na spana.
Source: JF
No comments:
Post a Comment