15 April 2015

NEWZZ!!:- WATU 9 WAKAMATWA NA POLISI MOROGORO WAKIWA NA VIFAA VYA KIGAIDI

Watu 9 wamekamatwa wakiwa wamejifungia kwenye msikiti wa Soni Morogoro wakiwa na vifaa vya milipuko hatari! Watu hao ni watanzania"!!

Katika purukushani hizo polisi mmoja amenusurika kuuawa baada ya kukatwa na jambia shingoni.



Name:  gaidi2.png
Views: 0
Size:  218.4 KB


Name:  Gaidi1.png
Views: 0
Size:  246.3 KB


Name:  gaidi3.png
Views: 0
Size:  231.1 KB


================

Quote By Standalone View Post
Watu 10 wakamatwa ‪msikitini‬ wakiwa na milipuko, sare za jeshi, 'bendera ya Al Shabaab'

Watu 10 wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro baada ya kukamatwa msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi na bendera nyeusi inayodaiwa kutumiwa na kundi la wapiganaji wa Al Shabaab wa nchini Somalia.

Katika tukio hilo, mmoja anayesadikiwa kuhusiana na watu hao waliokamatwa aliuawa na wananchi wenye hasira baada ya kumjeruhi kwa panga askari polisi aliyekuwa akipambana naye.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Leonald Paul alisema tukio hilo limetokea jana (Aprili 14 mwaka huu) majira ya saa 3.30 usiku katika kitongoji cha Nyandero, tarafa ya Kidatu wilayani Kilombero.



===updates===
Kamanda huyo alitaja vitu vilivyokutwa katika mabegi yaliyokuwa ndani ya msikiti huo ni pamoja na milipuko 30, bendera nyeusi yenye maandishi ya Kiarabu yakisomeka ‘Mungu Mmoja’, majambia, bisibisi, vinyago vya kuziba uso (masks), nguo za jeshi, misumeno ya chuma na spana.
 
 
Source: JF

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname