Kituo
kimoja cha televisheni nchini Marekani kinachorusha kila siku kipindi
cha mhubiri Pat Robertson kiliomba radhi Jumatatu kwa madai yake potofu
kwamba wasafiri wanaokwenda Kenya wanaweza kupata maambukizi ya Ukimwi
kwa njia ya taulo.
"Dr
Robertson alikosea kusema juu ya uwezekanao wa kupata Ukimwi kwa njia
ya mataulo," kimesema kituo cha Utangazaji cha Kikristo, CBN, katika
mtandao wa Facebook.
"CBN
imegundua mara moja kosa hili na kuondoa kauli hiyo kutoka kwa maktaba
ya mtandao huo. CBN inaomba radhi kwa mkanganyiko wowote."
Mhubiri
huyo mwenye umri wa miaka 84, mwinjilisti mkongwe ameonya katika
kipindi chake cha "700 Club" cha Oktoba 16 kwamba wasafiri watalazimika
kuchukua tahadhari ya hali ya juu ya kiafya wawapo nchini Kenya.

No comments:
Post a Comment