30 September 2014

PhD YA MIEZI MIWILI ALIYOPEWA MKE WA MUGABE YAWAKASIRISHA WANACHUO

Chama cha wanachuo nchini Zimbabwe, Ijumaa hii kimeutaka uongozi wa chuo kikuu cha Zimbabwe kujiuzulu baada ya kumpatia mke wa rais Robert Mugabe, PhD miezi miwili tu baada ya kuanza masomo.
Huchukua zaidi ya miaka mitatu hadi minne kwa mwanafunzi wa kawaida ili kupata PhD.
 PhD hiyo ilitolewa kwa Grace Mugabe, 49 aliyekuwa mpiga chapa wa zamani kwenye ofisi ya rais, wiki mbili zilizopita. Mke wa Mugabe alivalishwa kofia ya kuhitimu masomo hayo na mume wake pamoja na wahitimu wengine.
Utaoji wa PhD umetafsiriwa kama njia ya kifisadi ya kupandisha CV ya mke wa Mugabe ili aje kugombea urais pindi rais huyo akifariki.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname