02 August 2014

HATIMAYE MPENZI WA JOKATE MWOGELO AFAHAMIKA...NI HUYU HAPA MTANGAZAJI MAARUFU


Status ya uhusiano ya Jokate Mwegelo (kwa mujibu wake mwenyewe) inasomeka ‘single’ lakini huenda mambo yakawa yameshabadilika iwapo kile kilichopo katika mawazo yetu na yako baada ya kuona picha hizi kikawa ni kweli.
Nick Mutuma na Jokate Mwegelo Mjenzi wa ufa uliokuwa umebomoka kwenye moyo wa Jokate kutokana na mahusiano yake yaliyopita (Hasheem Thabeet na Diamond), anaweza akawa ameshapatikana. Naye si mwingine ni muigizaji wa kipindi cha MTV Shuga na mtangazaji wa redio, Nick Mutuma. Tangu aende Nairobi Kenya kikazi, Jokate na Mutuma wamekuwa karibu kiasi cha kuzalisha cheche za uwepo wa

uhusiano kati yao. Kupitia Instagram, Mutuma alipost selfie akiwa na mrembo huyo aliyemlalia kifuani kama msichana afanyavyo kwa boyfriend wake. Picha hiyo ilivuta macho na comments za wengi kwenye mtandao huo huku wengi wakisema wanapendeza kuwa pamoja. “I pray u b a couple..those kids u’ll get tho’ lol @nickmutuma , @jokatem,” ameandika mmoja na mwingine kuchombeza: That is one cuuuute couple aaaaaaww!!!! Jana pia Nick alipost picha hii ya TBT: Naye Jokate alipost picha ya Mutuma akiwa busy kwenye laptop na kuandika: #KenyanBoys always emoji @nickmutuma.”

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname