01 May 2014

RAY ASEMA YEYE NDIYO MSANII TAJIRI KULIKO WOTE HAPA BONGO, HAKUNA CHA DIAMOND, JIDE WALA MSANII YEYOTE ANAYEWEZA KUMFIKIA KWA PESA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjNbGXcRDIxCNZnJP6wrQD9ZLoRTsf_HKYecennO9uIy5YZkH4TnXRmsW_iKN0Nal4LjQ5CSpRZg1NzTe1al3ySMH7sQZ02A_yMUHGw1gdcEGwZw8aFU_N2ebFFNSIC3-VSukENBW8Vevc/s1600/IMG_0342.JPG
Star wa filamu nchini Vicent Kigosi "Ray" amesema kuwa yeye ana pesa na mali nyingi na hakuna msanii yeyote wa Tanzania awe wa filamu au muziki  anayemfikia sema hapendi tu kujitangaza kama baadhi ya mastaa wenzake akidai ni ulimbukeni. "hakuna msanii anayenizidi uwezo kuanzia mali na hata fedha niko mbali sana mimi, hata gari ninalotembelea hakuna msanii aliyenalo kama ingekuwa ni mtu wa kujisifusifu na kutafuta sifa za kijinga jamii ingejua" alisema star huyo wa filamu za Oprah, Sobbing Sound, Hard Price na Handsome Wa Kijiji akizungumza na gazeti moja.
 Ray vile vile aliamua kurusha kombora kwa wabaya wake wasiopenda maendeleo yake kwa kusema "wanaongea sana majungu,  fitina na vitu ambavyo havipo kuhusu mimi, mimi ni jembe, kwanini wasiangalie maisha yao? leo msanii unateta nae dakika hiyo hiyo anageuza maneno hayo kuwa majungu, acha nikae peke yangu nifanye issue zangu"

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname