24 May 2014

MWILI WA MAREHEMU AMINA NGALUMA WAWASILI DAR

Mwili  wa mwanamuziki Amina Ngaluma ukipokelewa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere ukitokea Thailand alipofia.
Jeneza lenye mwili wa  Amina Ngaluma likiwekwa kwenye gari tayari kupelekwa kwa mumewe Kitunda.

Mama mzazi wa Amina Ngaluma (kushoto) akilia kwa uchungu baada ya kuuona mwili wa mwanaye.
Waombolezaji wakijadili jambo.
Waombolezaji wakiwemo waandishi wa habari wakisubiri mwili wa marehemu Uwanja wa Ndege wa J ulius Nyerere Dar.
Jeneza lenye mwili wa Amina Ngaluma baada ya kupokelewa Uwanja wa Ndege Dar.
Mume wa marehemu Amina, Rashid Sumuni ambaye pia ni mwanamuziki akiwa na huzuni uwanja wa ndege wakati anasubiri mwili wa mkewe.
Msafara wa magari ukiondoka uwanjwa wa ndege wa kimataifa Dar na mwili wa marehemu Amina.
Baba wa marehemu mzee Kassim Ngaluma ( mwenye kofia) akiwa na huzuni wakati anasubiri mwili wa marehemu.
Mwanamuziki Cosmasi Chidumule (Katikati) akijadili jambo na wadau wa muziki akiwemo  Mzee Mbizo (kulia).
Gari lililobeba mwili wa marehemu.
Mwanamuziki Mwijuma Muumini akihojiwa na mwanahabari kabla ya maiti haijafikishwa uwanja wa ndege Dar.
Mwili wa marehemu Amina Ngaluma ukipokelewa uwanja wa ndege.
Waombolezaji wa msiba huo mmoja akilia kwa uchungu  wakati wa kuupokea mwili wa Amina Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar.
Shemeji wa marehemu ambaye ameoa mdogo wake na Amina Ngaluma akisubiri kuwasili kwa maiti Uwanja wa Ndege wa JK Dar.
Hatimaye mwili wa aliyekuwa mwanamuziki wa muziki wa dansi nchini Amina Ngaluma umewasili jana usiku jijini Da ukitokea nchini Thailand.
Mwili wa marehemu uliwasili kwa ndege ya  K.L.M  saa 4 kasoro robo  usiku wa jana, huku baadhi ya wadau wa muziki na wanandugu wakionesha kushangazwa na kitendo cha baadhi ya wanamuziki kutokufika katika kuupokea mwili wa Amina Ngaluma.
Kamera yetu ilishuhudia wasanii wachache waliowasili eneo la Uwanja wa Ndege akiwemo Mzee Cosmasi Chidumule na Mwijuma Muumini ambaye alitoka Kahama kwa ajili ya kuudhuria mazishi ya mwanamuziki huyo anayetarajiwa kuzikwa leo mchana.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname