04 April 2014

JOHARI: NIPO RJ SIKO NA RAY

MUIGIZAJI wa ‘long time’ katika tasnia ya filamu Bongo, Brandina Chagula ‘Johari’ juzi kati amefunguka kuwa kwa sasa hayuko na aliyekuwa akidaiwa kuwa ni mpenzi wake, Vicent Kigosi ‘Ray’ ila yuko katika Kampuni ya RJ ambayo wanashirikiana kisanii zaidi. 
Muigizaji wa Tasnia ya filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’
Akizungumza na Ijumaa katika hoteli ya Johannesburg, Sinza Mori jijini Dar, Johari alisema kuwa kwa sasa angependa atambuliwe kuwa anafanya kazi na Ray katika hiyo kampuni na si kuhusishwa naye kimapenzi.
“Naomba ifahamike kwamba mimi niko RJ na siko na Ray kama watu wengi wanavyozungumza,” alisema Johari kwa kifupi kisha kuendelea na hamsini zake.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname