Ni mara ya
kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya
Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili
alikokuwa amelazwa.Hakika @Ufoo Saro aliokoka kuuliwa mwaka jana
mwishoni@
Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT)
Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo huku akitokwa na machozi
na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu
yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”
Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote alichokuwa mgonjwa.
“Sina
cha kuwalipa, ninawashukuru sana kwa wema wenu, pia kwa kuniombea.
Mungu ni mkubwa na amenipigania, naendelea vizuri kwa sasa,” alisema na
kuongeza:
“Mungu
alinisimamia na nyinyi pia mliniombea, hakika sina budi kushukuru kwa
kila jambo. Nitasoma zaburi ya 146 katika Biblia Takatifu ili kumshukuru
Mungu kwa kunisaidia.”
Ufoo alisema kuwa ameamua kumshukuru Mungu kwa sababu siyo watu wote wanaopata matatizo kama yake wanapona.
Mchungaji aliyeongoza misa hiyo iliyoanza saa 1 asubuhi hadi saa 5 asubuhi,Joseph Maseghe alisema Mungu hakupanga Ufoo afariki dunia kwa kupigwa risasi.
“Mungu
bado anakuhitaji, hakupanga ndiyo maana upo nasi leo. Hautakiwi kulia
huu ni mwanzo wa maisha yako mengine, usilie unachotakiwa ni kumshukuru
Mungu kwa kila jambo,” alisema

Mchungaji Maseghe, elewa kwamba kulia kwake hakuna maana hamshukuru Mungu bali anatoa bubujiko la moyo wenye shukrani za dhati kwa Mungu toka kina cha ndani cha moyo wake kwa matendo makuu Mungu ametenda. Kulia pia relief ya kile kilichosibu moyo wa mtu na kumfanya mtu ajerejee kwenye hali yake ya uimara. Ufoo ni halali alie kwa sababu hata kusimama mbele za Madhabahu ya Mungu si kitu cha mchezo. Tunalia kwa Mungu kama sehemu ya majuto ya mambo mengi mabaya yaliyotukumba.Chozi ni jutio na ni toba ya hali ya juu kabisa kujililia nafsi yako.Mungu akulinde na kukupa moyo wa ujasiri kuhakikisha unaongezeka imani zaidi katika hayo yaliyokutokea umjue zaidi Mungu.
ReplyDelete