25 December 2013

INAUMA SANAA RAFIKI YANGU ANATEMBEA NA MAMA YANGU MZAZI..NAOMBENI USHAURI NIFANYEJE

Hii imetokea wiki kadhaa zilizopita.
Kijana mmoja jirani yangu ana rafiki yake. Walikuwa wanasoma pamoja. Ni marafiki wakubwa ambao hata wazazi wanajua. Walikuwa wanasoma pamoja na kushirikiana mambo mengi.

Kijana kaenda shule hakumkuta rafiki yake. Kuuliza akaambiwa anaumwa. Kwa mapenzi aliyo nayo kwa rafiki yake akaamua arudi nyumbani abadili nguo ili akamtembelee rafiki yake mgonjwa.
Hapo ndipo alipokutana na zahama. Rafiki yake yuko juu anammega mama yake mzazi, tena sebuleni kwenye kochi! Kijana hakuamini macho yake, kwamba rafiki yake mpenzi anammegea mama yake mzazi!! 

Akatoka mbio mpaka kwa uncle wake kumweleza dhahama hiyo. Uncle kajaribu kuweka mambo sawa imeshindikana. Mama kanogewa, kijana kanogewa. Hivi sasa ni kama wameoana, mtaani wanarandaranda na gari ya mama yake rafiki yake, kijana dereva mama abiria! Wala si siri tena

Kijana wa watu amegoma kurudi nyumbani, rafiki yake amemsaliti. 


Amehamia kwa uncle wake. Kinachomuumiza kichwa zaidi ni kuwa dada zake wawili wanamuunga mkono mama yao. Hawaoni tatizo liko wapi wakati baba yao alishafariki na mama anahitaji pumziko.
Anachotaka sasa ni ushauri, alipe kisasi au asahau aendelee na hamsini zake?


Na kama ni kulipa kisasi, alipeje? Kijana wa watu amechanganyikiwa hata maendeleo yake darasani yameshuka sana.

Wanajamii changieni mawazo jinsi ya kumshauri kijana huyu asizidi kuathirika

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname