FLORA MVUNGI ATELEKEZA KICHANGA USIKU MNENE NA KWENDA KULA BATA..!!
LICHA ya kuwa na kichanga, staa wa filamu za Kibongo, Flora Festus
Mvungi amenaswa usiku wa manane ‘akila bata’ jambo lililozua mshangao
kwa wadau waliokuwepo eneo hilo.
Msanii
huyo alinaswa na ‘kiranja’ wa gazeti hili hivi karibuni ndani ya Ukumbi
wa Vijana Social, Kinondoni jijini Dar kulipokuwa na tamasha la vipaji,
alipofotolewa picha, aling’aka!.
“Sitaki picha bwana, wewe hujui kama nimetoroka usiku huu kuwa hapa!
Naomba ufute hizo picha tafadhali, usiniudhi bwana,” alisema Mvungi huku
akikwepa miale ya kamera.
Source: GPL
No comments:
Post a Comment