20 August 2013

Mambo si mazuri tena kwa waafrika nchini malaysia – mdau

Uncle michuzi asante kwa kuweka ile habari juzi ya kukamatwa mtu na madawa ya kulevya mwenye pasipoti ya Tanzania. 
Sasa after the incident ya watu ambao kwa 100% tuna uhakika ni wanigeria kukamatwa na sembe na wengine kua involved kwenye cases tofauti zikiwemo human traficking and prostitution sasa wamilik wa condominiums (aina ya hosteli) mbali mbali zinazomilikiwa na Ridzuan Properties wamepitisha utaratibu huu ya kwamba hawataki tena waafrika kukaa kwenye nyumba zao. 
Hivyo mzazi mwenye mpango wa kumleta mtoto wake huku au mwanafunzi mwenye mpango wa kukaa na  kusoma huku especially Taylors university, Sunway university, Inti university na Segi college Subang tunawashauri ku-book hostel za chuo mapema wasitegemee kukaa nje ya hostel.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname