Jengo la
Bakwata lililopo kwenye makutano ya Barabara ya Morogoro na Bibi Titi
jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia juzi lilibolewa ghafla wakati
mali za wapangaji zikiwemo ndani na kusababisha hasara kubwa ya
uharibifu na upotevu wa mali. Chanzo kimoja cha habari eneo hilo kimedai
kuwa Bakwata wamelibinafsisha jengo hilo kwa mwekezaji kutoka nje ya
nchi bila kuwashirikisha wapangaji wake. Mwekezaji huyo ndiye anayedaiwa
kutoa agizo la kubomoa jengo hilo kabla ya notisi aliyoitoa kwa
wapangaji hao kumalizika.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)




No comments:
Post a Comment