![]() |
| HUYU NDO MWANAMKE ALIYE UWAWA HAPA ENZI ZA UHAI WAKE |
Pistorius alikuwa mwanariadha wa kwanza mlemavukushiriki michezo ya olympic
Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amekamatwa na polisi na amekuwa akihojiwa kuhusu mauaji ya mpenzi wake nyumbani kwake mjini Pretoria.
Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, amekamatwa na polisi na amekuwa akihojiwa kuhusu mauaji ya mpenzi wake nyumbani kwake mjini Pretoria.
Kulingana na vyombo vya habari, mkuu wa polisi,
Sarah Mcira, aliambia wanahabari kuwa mwanamke aliyefariki nyumbani kwa
mwanariadha huyo alipigwa risasi kwenye mkono wake na kichwani.
Hata hivyo hali iliyosababisha mauaji hayo bado haijulikani.
Duru zinasema kuwa Pistorius huenda alimuua Reeva Steenkamp kimakosa kwa kudhania kuwa ni mwizi aliyekuwa amemvamia.
Polisi wanasema wamemkamata mtu mwenye umri wa
miaka 26, lakini hakuna thibitisho lolote kuwa ni Pistorius.Mshukiwa
anatarajiwa kufikishwa mahakamani baadaye leo.
Pia ilithibitishwa kuwa mwanamke mmoja aliuawa
nyumbani kwa Pistorius na kwamba alikuwa rafiki yake. Polisi walisema
kuwa awali kulikuwa na visa kadhaa vilivyoriptiwa kutokea katika sehemu
anakoishi Pistorius na kutajwa kuwa madai ya unyanyasaji au dhulma za
kinyumbani.
Pistorius anasifika kama mwanaridha wa kwanza
mlemavu kushiriki michezo ya Olimpiki. Habari za mauaji ya mpenzi wake
Pistorius zimewashangaza wengi Afrika Kusini kwani anasifika kama
mwanaridha anayeiletea nchi hiyo sifa.
Afrika Kusini ni moja ya nchi zenye visa vingi vya uhalifu duniani na watu wengi wanamiliki silaha za kujilinda.
