28 February 2015

YANGA YAKUBALI KICHAPO CHA WANAJESHI

Timu ya klabu ya Yanga imefanikiwa kufuzu hatua nyingine ya mtoano katika mashindano ya kombe la shirikisho pamoja na kukubali kipigo cha magoli 2 - 1 dhidi ya BDF XI.


pambano hilo lililopigwa Botswana katika uwanja wa Lobatse lilikuwa la kuvutia na wenyeji walijaribu kushambulia ili kupata magoli kwani tayari walikuwa nyuma kwa magoli 2 - 0.

Wenyeji walianza vibaya pambano hilo kwani katika dakika ya 20 mchezaji wao Othusitse Mpharithe alioneshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mbaya Simon Msuva.

Alikuwa ni Mrisho Ngassa aliyeandika bao la kwanza dakika ya 29 baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira mzuri aliopigiwa na Amissi Tambwe.

dakika ya 49 BDF walipata bao kupitia kwa Msimonyane. Na baadaye dakika ya 85 walipata bao la 2 kupitia Kulumbani.

Kwa matokeo hayo Yanga wanafuzu hatua nyingine kwa ushind wa jumla wa magoli 3 - 2.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname