19 November 2014

SINA MAHUSIANO NA SITTI MTEMVU - LUNDENGA ASEMA




0




Mkurugenzi wa Lino Agency akichat Live na mashabiki wa EATV kupitia ukurasa wa facebook wa EATV
Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ni waandaaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mahusiano ya kimapenzi na aliyekuwa mshindi wa kwanza wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu.Lundenga amefunguka hayo leo alipokuwa akichata Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa sita mchana mpka saa nane mchana.
Mbali na mahusiano Watu wengi walitaka kujua ni sifa zipi zilizompelekea mrembo Sitti Mtevu kutwaa taji hilo kama si upendeleo kutoka katika kamati na crew inayohusika kuandaa mashindano hayo kwani watu wengi wamekuwa wakisema kuwa mrembo huyo alikuwa hastahili kushinda taji hilo ukilinganisha na warembo wengine ambao walikuwa wakichuana nae,kufuatia hali Ludenga ikabidi aweke wazi sifa tano amabzo zinamfanya mtu kushinda taji la Miss Tanzania kuwa ni lazima awe na sura nzuri, umbo zuri, mvuto, haiba, ufahamu wa kutosha wa mambo mbali mbali.SOMA ZAIDI>>>

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname