MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha DTV, Peniel Mungilwa ambaye
ni zilipendwa wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond
Platnum’ amesema katika maisha yake haitatokea akamdharau kwa kumkashifu
hata kama si wake tena.
Akipiga stori na paparazi wetu, mwanadada huyo alisema japo kwa sasa
ametofautiana na Diamond aliyeweka wazi kwamba yupo na Wema Sepetu
hawezi kuwa na chuki dhidi yao.
“Naapa kwa Mungu wangu katika maisha yangu haitatokea kamwe
nikamdharau Diamond, haijalishi yupo na nani kwa sasa, thamani yake
kwangu itabaki palepale hamuwezi jua namheshimu kiasi gani yule mtu,”
alisema Penny.
No comments:
Post a Comment