07 April 2012

Chadema watangaza kukata Rufaa Mahakama Kuu ya Rufaa Tanzania

Rufaa hiyo wanataraji kuikata hivi karibuni katika Mahakama kuu ya Rufaa Tanzania. 
Wakihutubia umati mkubwa wa wakazi wa Arusha na viunga vyake waliofruka katika viwanja vya NMC, mapema leo viongozi hao akiwepo Godbless Lema mwenye aliwasihi wananchi kuendelea kuwa watulivu na kuondoa hofu na anaimani watashinda.

Mahakama Kuu  Kanda ya Arusha ilitoa hukumu hiyo na kutengeua Ubunge wa Godbless Lema baada ya kumkuta na hatia ya kutumia lugha ya udhalilishaji na maneno ya kashifa dhidi ya mgombea wa  Balozi Dk. Batilda Buriani katika uchaguzi wa mwaka 2010 alipokuwa akigombea kwa tiketi ya CCM.

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho Freeman Mbowe alisema zipo sababu tatu zilizowafanya waende kukata Rufani badala ya kuingia kwenye uchaguzi mdogo moja kwa moja.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname