SERENGETI BREWERIES LTD

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
DEREVA AJISHINDA MTOKO WA MBUGANI KATIKA PROMOSHENI YA TUTOKE NA
SERENGETI
Tarehe 23/12/2014, Dar es Salaam,
Bw.
Deogratias Peter Masenga mwenye umri wa miaka 24 ambaye ni dereva wa malori
makubwa na mkazi wa mkoa wa Kilimanjaro atasherekea sikukuu ya krismasi kwa
staili ya aina yake baada ya kuibuka mshindi wa safari inayogharamiwa na SBL
kupitia kampeni yake inayojulikana kama ‘Tutoke na Serengeti’.
Deo alitangazwa
mshindi katika safari ya “MTOKO WA MBUGANI” kupitia droo ya kawaida ya kila
wiki iliyofanywa katika ofisi za Serengeti katika mazingira ya uwazi na kushuhudiwa
na vyombo vya habari mbalimbali, Price Water Coopers (PWC) na maafisa kutoka
Bodi ya Bahati Nasibu ya Taifa.
Akizungumza
kwa njia ya simu akiwa Moshi mjini kwa shughuli zake za kikazi, Bw, Deo ambaye alijawa
na bashasha mara baada ya kupata taarifa hizo alisema “Hii ni mara yake ya kwanza
kushinda kitu cha namna hii. Nina furaha sana kuibuka mshindi, hakika naumaliza
mwaka kwa staili ya aina yake nawashukuru sana Serengeti”.
Deo ambaye
alimchagua kaka yake kama mtu wa kwenda naye kwenye safari hiyo, aliwashauri
watu wengine wasikate tamaa na kujaribu kushiriki mara kwa mara katika
promosheni hii .
Kwa upande
wake, Kaimu Meneja wa Bia ya Serengeti, Bw. Elihuruma Ngowi alisema …”Kampuni
ya Serengeti itatumia kiasi cha shilingi za kitanzania milioni 10 kwa ajili ya safari
ya mshindi na anaruhusiwa kwenda na mwenza au mtu yeyote atakaye mpendekeza kwenye
mtoko huu wa siku mbili katika mbuga ya wanyama ya Serengeti…. Kiasi
kilichotajwa kitawawezesha kupata fedha za kujikimu, malazi, usafiri na mambo
mengine,” aliongeza Elihuruma
Bw. Elihuruma
alisisitiza kwamba promosheni hiyo bado inaendelea na milango ipo wazi kwa
wateja wote na kuwaomba waendelee kujitokeza kushiriki “Bado kuna washindi
watatu watakaoshinda safari hii ya Serengeti, kwa hiyo nachukua fursa hii
kuwatia moyo wateja wote wa Serengeti kuendelea kushiriki kwenye promosheni hii
ya aina yake”.
Ili kuweza
kushiriki kwenye promosheni hii wateja wanatakiwa kununua bia ya Serengeti
Premium Lager na kuangalia ndani ya vizibo na kuna namba ambazo wanapaswa
kuzituma kupitia ujumbe wa simu za mkononi (sms) kwenda 15317 na moja kwa moja
wataingia kwenye droo na kuweza kushida zawadi kama vile Limo Bajaj, Pesa
Taslimu, Punguzo la shilingi 300 kwenye bia na bia za bure na unavyozidi kutuma
namba hizo kutoka kwenye vizibo ndipo unapojihakikishia nafasi ya kushida.
Kwa Taarifa zaidi Tembelea.
Tembelea
kurusa za facebook na twitter za Serengeti Premium Lager
ABOUT SERENGETI BREWERIES LIMITED
Serengeti
Breweries Limited engages in the brewing, manufacturing, marketing and selling
drinks made of malt, hops and barley and sorghum in Tanzania.
Headquartered in Dar es Salaam, SBL brands include:-
Serengeti Premium Lager, Serengeti Platinum, Tusker Lager, Tusker Lite, Kibo
Gold, Uhuru Peak Lager, Pilsner Lager, Senator, The Kick and Guinness®.
SBL is also the sole distributor of several
international renowned spirits including Smirnoff Vodka®, Johnnie Walker®,
Bailey’s Irish Cream ®, Richot®, Bond 7 Whiskey® and Gilbeys Gin®.
Serengeti Breweries Limited is a subsidiary of
East African Breweries Limited/ DIAGEO PLC.
No comments:
Post a Comment