01 August 2014

Mama Wema Sepetu Aanza Kumkubali Diamond Platnumz, Wema Ajawa Na Furaha.


Wema na mama yake mzazi
Baada ya Mariam Sepetu ambaye ni mama mzazi wa Wema Sepetu kutokumkubali Diamond Platnumz kama mpenzi wa mwanae hatamaye mama Wema ameanza kumkubali Diamond. Akizungumza na Globalpublishers Wema amesema kuwa kwa muda mrefu alikuwa hana maelewano mazuri na mama yake sababu ya uchumba wake na superstar huyo wa Bongofleva lakini kwasasa ameanza kumkubali

"Mama nilikuwa nikimsihi sana juu ya uchumba wangu na Diamond lakini sasa tumefikia hatua nzuri namshukuru Mungu amekubali, maana siku hizi nikionana naye ananiuliza vipi mwenzako mzima, anaendeleaje, wakati mwanzoni haikuwa hivyo" alisema Wema

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname