30 August 2014

Hivi ndivyo hali ilivyokuwa Serengeti soka bonanza-Moshi

Mchezaji wa Timu ya Mandela, John King akimtoka Ismail Fundi wakati wa  shindano la Serengeti Soka Bonanza lililofanyika katika viwanja vya Moshi klabu leo ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za tamasha la Serengeti fiesta linalotarajiwa kufanyika kesho Jumamosi mjini Moshi.

Nahodha wa timu ya Mandela Bar, Salehe Senkunde (kushoto) akipokea sehemu ya sanduku tano  za bia ya Serengeti kutoka kwa Meneja Masoko Kanda  ya Kaskazini, Patriki Kasaka, (kulia) baada ya kuibuka washindi wa pili katika kinyang’anyiro cha  Serengeti soka bonanza  katika Viwanja vya Moshi klabu. Timu tano zilishiriki  bonanza hilo.


Meneja wa Timu ya Moshi klabu, (kushoto) akipokea kikombe na sehemu ya sanduku kumi za bia ya serengeti toka kwa Meneja Masoko wa  Bia  ya Serengeti,  Allan Chonjo, (kulia) mara baada ya timu hiyo kuibuka mshindi wa Serengeti Soka bonanza katika mashindano yaliyofanyika katika Viwanja vya Moshi klabu mjini Moshi

wanachama wa timu ya Moshi klabu wakifurahia ushindi wao baada ya kujishindia sanduku kumi za bia ya serengeti.  jumla ya timu tano zilichuana katika kinyang’anyilo hicho cha Serengeti.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname