27 August 2014

ASHAMBULIWA NA RAIA KISHA KUFA BAADA YA KUIBA SIMU MBEYA


Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Frank Mwakilalo (25) mkazi wa Block T alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Mbeya baada ya kupigwa na kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi kwa tuhuma za kuiba simu.
Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 02:15 usiku huko katika maeneo ya Block T, jiji na mkoa wa Mbeya. Inadaiwa kuwa marehemu alikamatwa na kuanza kupigwa na wananchi hao na badae alipelekwa na kufungiwa katika ofisi za mtendaji ambapo alitoroka na ndipo wananchi hao walimuona na kumkimbiza na kuanza kumpiga hali iliyopelekea kumvunja mkono wake wa kushoto na kumsababishia maumivu makali mwilini.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname