16 August 2013

TAMKO LA VIONGOZI WA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAMU BAADA YA KUTOLEWA HOSPITALI SHEIKH PONDA

Msemaji wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Rajan Katimba (katikati) akiongea na wanahabari..SOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Wanahabari wakiwa kazini wakati wa mkutano huo.
Polisi wakidumisha ulinzi nje ya msikiti wa Mtambani ambapo mkutano umefanyika.
Mjumbe kutoka Organization of Scholers in Tanzania, Ally Basalleh naye akiongea wakati wa mkutano huo.
Wanajumuiya hao wakinena mara baada ya mkutano huo.
Taarifa iliyotolewa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini.
Viongozi wa  Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, leo wamekutana na wanahabari katika msikiti wa Mtambani Kinondoni jijini Dar, kujadili juu ya kutolewa hospitali katibu mkuu wa jumuiya hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda. Sheikh Ponda alichukuliwa na polisi kutoka katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI) jana majira ya saa nne na nusu asubuhi. Katika taarifa yao waliyoitoa kwa wanahabari, viongozi hao wamelaani kitendo hicho alichofanyiwa Sheikh Ponda na kuitisha mkutano wa dharura utakaofanyika Jumapili ya Agosti 18 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri katika Viwanja vya Nuruh Yakin Temeke jijini Dar es Salaam ili kutafakari kwa pamoja na kuchukua hatua.
(PICHA NA DENIS MTIMA / GPL)

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname