23 December 2013

KATISHAAAA MBAYAAA....CHEKI ADEBAYO AKICHEZA NGOLOLO LIVE BAADA YA KUFUNGA BAO

Jana, Emmanuel Adebayor aliwakumbusha mashabiki wake kuwa linapokuja suala la kucheza, kuna mshindi mmoja pekee – yeye. Tottenham iliibuka na ushindi wa mabao 3 kwa 2 dhidi ya Southampton ambapo mawili aliyapachika wavuni mwenyewe.
adebayor

Adebayor akicheza mbele ya refa Chris Foy aliyeonekana kutofurahishwa na uchezaji wake
Kwa baadhi ya watu uchezaji ule umefananishwa na mtindo ulioanzishwa na Diamond Platnumz, Ngololo Dance kwenye video yake ya My Number One.
adebayor 2
“Adebayor just did that dance u do “number one” after scoring,” aliandika mfuatiliaji wa mechi hiyo ya jana.
Diamond naye aliamua kumshukuru Adebayor waliyekutana naye hivi karibuni nchini Nigeria kwenye harusi ya Peter Okoyo wa P-Square ambako alimuonesha jinsi ya kucheza Ngololo Dance.
‘Das ma Brother @sea25 …. Appreciate so much king…. SALUTE,’ aliandika Diamond kumshukuru Adebayor.
Hata hivyo wengi wamepinga mchezaji huyo kutumia uchezaji wa Ngololo na kwamba mara zote hucheza hivyo.’Ile style anacheza tangu yupo arsenal bwan co ngololo cc mashabik wa arsenl tunmjua yule,’ ameandika shabiki mmoja.

Katika hatua nyingine Adebayor ameishutumu Tottenham kwa kumkosea heshima. Mchezaji huyo mwenye miaka 29 hakujumuishwa kwenye picha rasmi ya pamoja ya club hiyo na alikuwa akifanya mazoezi mwenyewe kipindi Andre Villas-Boas alikuwa meneja.
“Ilikuwa ngumu,” alisema Adebayor. “Nilipokuwa naenda mazoezini na kuona picha ya timu ambayo mimi sikuhusishwa, hiyo ilionesha kukosewa heshima kwa kiasi kikubwa.”
Adebayor alikaa msimu mzima kwa mkopo akiwa na Tottenham akitokea Manchester City mwaka 2011-12 kabla ya kujiunga na Spurs kwa mkataba wa £5m August 2012.
Credit-Bongo5

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname