27 January 2016

Yasome hapa maamuzi ya kamati ya uongozi kuhusu hoja ya Zitto

Baada ya Bunge kurejea jioni hii mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge ameliambia Bunge kuwa maamuzi ya kamati ya uongozi baada ya kuketi mchana wa leo ni kama ifuatavyo.

(a) Mwenyekiti wa Bunge alikuwa sahihi kutaka hoja iliyokuwa mbele ya Bunge kuhusu hotuba ya Rais iendelee.
(b) Hakuna haki yoyote ya Bunge iliyovunjwa kwa Bunge kuendelea na kazi yake baada ya kauli ya waziri
(c) Hoja ya Bunge iliyo mbele ya Bunge ni hotuba ya Rais na kamati ya uongozi imeagiza shughuli ziendelee kama kawaida.
(d) Endapo kuna mbunge yoyote ambaye hataridhika atumie kanuni ya 5 (4) kuomba kibali kwa katibu wa bunge ili apate nafasi maalum.
Aidha kwa mujibu wa ratiba ya kikao cha Bunge ni kwamba Bunge litajadili hotuba ya Rais Magufuli aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 11 Novemba 20, 2015 kwa muda wa siku 3

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname