DAR
ES SALAAM: Yamekwisha! Baada ya kudumu ndani ya bifu kwa muda mrefu
huku wakituhumiana uchawi, hatimaye mwigizaji Aunt Ezekiel na mzazi
mwenzie na Moses Iyobo, Mwengi Ally wamekutana na kumaliza tofauti zao.
Mapema
mwaka jana, wawili hao waligombana kufuatia Iyobo ambaye ni dansa wa
staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kummwaga Mwengi
kisha kuanzisha uhusiano na Aunt ambapo uhusiano huo ulijibu na
wakafanikiwa kupata mtoto.
Aunt
ndiye aliyeamua kufuta ‘kinyongo chao’ ambapo alisema hakuona sababu ya
wao kuendeleza bifu lisilokuwa na msingi wowote na kuwa wao ni wazazi
na watoto wao ni ndugu wa damu moja, alimshauri Iyobo awakutanishe,
wamalize tofauti zao.
Baada
ya kukubaliana, Aunt na Mwengi walikutana katika Hoteli ya Girrafe
iliyopo Mbezi Beach, jijini Dar wakiwa na Iyobo ambaye alisimamia zoezi
zima la mapatano kwa wawili hao kuzungumza, wakaelewana, ‘wakazika’
tofauti zao na kila mmoja kubeba mtoto wa mwenzake kisha kula na kunywa
pamoja.
Akizungumzia
tukio hilo la kiungwana baada ya Risasi Jumamosi kumtafuta, Aunt
alisema:“Unajua sisi ni wazazi na tuna watoto kwa baba mmoja (Iyobo),
kuendeleza mabifu ambayo hayana msingi siyo kitu kizuri tunatakiwa
kuwafundisha watoto wetu upendo siku zote, ndiyo maana tumeyamaliza,”
alisema Aunt.
Kwa upande wa Mwengi, alisema:
“Hakuna
jambo lisilokuwa na mwisho vitu vingine ni vya kupita katika maisha ya
sasa hivyo ni bora kuweka mabifu pembeni ili kuruhusu baraka,” alisema
Mwengi.
Wawili
hao walikubaliana kuwa muda wowote Mwengi atakuwa akimpeleka mtoto wake
nyumbani kwa Iyobo (baba’ke) na baadaye atakapofikisha umri wa kuanza
masomo, atamhamishia nyumbani anakoishi Iyobo na Aunt ili wamlee pamoja
na mtoto wa Aunt.
Kabla ya kupatana huko, Mwengi alimtuhumu Aunt kuwa ni mchawi.
No comments:
Post a Comment