16 January 2016

MASIKINI STARTV,REDIO UHURU,REDIO FREE AFRIKA,KISS FM, TCRA YAZIFUNGIA RASM VIPO PIA NA VITUO VINGINE 24 VYA REDIO NA TV,NI KILIO TU,SOMA HAPO KUJUA

 
MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA) imevifungia vituo 21 vya redio pamoja vituo sita vya Television kwa mda wa miezi mitatu baada ya kushindwa kulipia ada ya reseni.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
   Akithibitisha kufungiwa  Vituo hivyo vya habari leo jijini Sar es Salaam wakati alipokuwa anazungumza na fullhabari.blogs,Afisa Habari wa (TCRA) Bwana Mungi amedema kuwa Mamlaka hiyo imefikia hatua hiyo, baada ya vituo hivyo kukiuka sheria ya Utangazaji na Posta ya Mwaka 2014 ambayo inavitaka vituo hivyo kulipia ada ya Reseni ya Matangazo kwa kila mwaka na ada  ya masafa.
“Kifungu cha 22 cha sheria ya EPOKA ambayo ipo sura 306 na kifungu cha 21(g) inasema kuwa kampuni inaposhindwa kulipia ada ya reseni inapewa siku 30 ili aweze kulipa lakini hawa tumewapa taarifa lakini wamekaidi na wengine wanadaiwa tangu mwaka jana,kwahiyo ,sheria inasema wazi na sisi tumewapa notsi ya siku 30 na bado wakawa wanasuasua kulipa, Tumevifungia kwa miezi mitatu”Amesema  Mungi. 
Mungi avitaja vituo hivyo vya Redio vilivyofungiwa  ni Redio Uhuru,Redio Free Afrika,Kiss Fm,Ebon Fm,Redio Five,Country FM,Generation Fm,Impact Fm,Kill Fm,
     Vyengine ni Local Fm redio,Prive Fm,Court Fm, Sibuka FM,Standard Fm,Ulanga FM, Kifimbo,Tull Fm,Pride Fm,Redio Uhuruma,Redio Sengerema,
    Hata hivyo,Mungi alizitaja  pia vituo vya Television sita ambavyo vimefungiwa ni StarTv,Iringa TV,Mbeya TV,Mussa Tevesion Network,Tanga Tv,Sumbawanga Tv.
  Mungi ameongeza kuwa vituo hivyo vimetakiwa kuzima matangazo yake kwaanzia usiku wa jumapili ya terehe 17 ya mwezi huu,  na endapo kituo chochote kikaidi basi kitachukuliwa hatua kali za sheria.
     Hata hivyo,Mungi amesema endapo kituo cha chochote kitakacholipa ndani ya miezi mitatu kwenye kifungo hicho kitafungiliwa.
“Katika kipindi cha miezi mitatu kituo chochote kikilipa ada ya resini ,na akatimiza matakwa yote ya kisheria na akalipa pesa zote anazodaiwa basi sisi tutamfungulia”amesema Mungi,
Vilevile Mungi amedai kuwa endapo miezi mitatu ya kifungo hicho ikipita na vituo hivyo vitashindwa kulipa ada ya reseni basi Mamlaka hiyo itavinyang’anya reseni ya utangazaji na kuamuliwa kuanza upya kuomba reseni.
   WADAU WA HABARI WANENA.
Wakizungumza na Fullhabari.blogs wadau mbali mbali wa habari nchini wamesema hatua ya TCRA kuvifungia Vituo hivyo ni jambo la hatari katika ukuwaji wa sekta ya habari.
“Hapo TCRA inabidi waangalie vizuri,maana sekta ya habari Tanzania ni ngumu sana tofautisha na nchi ya Kenya,wenzetu wale wanaviwanda vingi sana,viwanda vile vinapeleka bidhaa kwenye vyombo vya habari kutangaza na redio zinapata pesa,sasa hapa nchini hakuna viwanda kwahiyo media zinang’ang’ania matangazo tigo,voda tu,wewe unategemea nini,vitakufa vingi tu”amesema Jackson Maliasi Msomi wa masuala ya habari kutoka chuo kikuu huria

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname