20 July 2015

HIZI NDO PICHA ZA MAJAMBAZI WALIO FANYA TUKIO LA MAUAJI YA POLISI NA RAIA KITUO CHA STAKISHARI DAR ES SALAAM


Hii  ni story nyingine kutoka kwenye ile ishu ya kuvamiwa kwa kituo cha polisi cha stakishari Jijini Dar es salaam ambapo askari wane na wananchi waliuawa na wale waliotambulika kama majambazi na kupora silaha kadhaa na kutoweka nazo.

Leo kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam alijitokeza mbele ya wanahabari na kuja na mafanikio ya msako mkali unaoendeshwa na jeshi la polisi ambapo hadi sasa majambazio watano wamekamatwa huku watatu kati yao wakiwa wameuawa na jeshi la polisi,huku silaha zilizoibiwa kukutwa katika maeneo ya mkuranga zikiwa zimefukiwa chini tayari kwa ualifu.

Sasa pamoja na mafanikio hayo polisi wanasema kuwa bado kuna majambazi waliohusika na lile tukio hawajakamatwa na kuna silaha nyingine bado hazijakamatwa,bahati nzuri jeshi la polisi limefanikiwa kukamata majina na picha za hao ambao bado hawajakamatwa.
Majina yako hapa kama picha juu zinavyoonyeshwa na kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es salaam

MAJINA YA MOST WANTED

1-ABDULAZIZI AHMAD ABDULRASHID maarufu kama USTADH ABDULAZIZI anaishi jijini Dar es salaam na ndiye kiongozi wa kundi hilo la wahalifu.

2-SHABAN MOHAMED MTUMBUKA maarufu kama AMIR SHABAN NDOBE

3-HANNAFI JUMANNE KAPELA

4-HASSAN HAROUNA ISSA maarufu kama DR SHUJAA

5-ZAHAQ RASHID NGAI maarufu kama MTU MZIMA

6-ABUBAKAR NGINDO maarufu kama ABU MUHAMMAD

7-KHAMIS RAMADHAN
Jeshi la polisi linaomba popote uonapo hizi sura wajulishe polisi popote ulipo.

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname