29 July 2014

CHEKI IDADI YA TUZO ALIZO NAZO DIAMOND PLATNUMS

mwanamuziki Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz

BAADA ya kuzikosa tuzo za MTV Africa na BET, hatimaye mwanamuziki Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, usiku wa kuamkia jana Jumapili ametwaa tuzo mbili kupitia African Music Magazine Awards au AFRIMMA zilizotolewa huko Texas, Marekani.
Diamond ametwaa tuzo mbili za Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki na ya Wimbo Bora wa Kushirikiana.
Baada ya kutwaa tuzo hizo, Diamond amerudisha shukrani zake kwa Rais Jakaya Kikwete akisema ndiye aliyempa nguvu ya kufanya muziki kwa ari kutokana na mchango wake kwa sanaa nchini.
“Nakushukuru sana Rais Kikwete kwa mchango wako, kijana wako nimefanya maajabu, lakini hii yote imetokana na mchango wako kwa wasanii nchini, baada ya kiongozi wetu kuonyesha kuijali kazi yetu na sisi imetupa moyo wa kufanya makubwa zaidi,” alisema.
Tuzo nyingine ya Diamond ni ile ya Wimbo Bora wa Kushirikiana ambao ni ‘Number One remix’ alioufanya na Davido wa Nigeria. Hata hivyo nyota huyo alisema ushindani uliopo sasa umemsaidia kwa kiasi kikubwa kufika alipo na anaamini kwamba imetokana na michango ya watu wengi.
“Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu, mama, familia, uongozi wangu, kipenzi changu, vyombo vya habari bila kuwasahau mashabiki wangu kwani siku zote wamekuwa wakiniunga mkono kwenye shida na raha na pia wasanii wote wa ndani na nje ya Tanzania kwani changamoto tunazopeana ndizo zilizotufikisha tulipo,” alisema Diamond.
Naye Meneja wa Diamond, Babu Tale aliyeambatana naye Marekani alisema tuzo hizo ni ushindi mkubwa kwa Tanzania kwani wamewapita wasanii waliokuwa wakiogopwa.
“Hii inadhihirisha tunaweza na tutafika mbali, tumewashinda Mafikizolo, 2Face na wengine wengi. Tupo mbali na ni hatua nzuri kwa muziki wa Tanzania,’’ alisema Babu Tale.
Nyimbo zilizokuwa zikiwania tuzo ya ‘kolabo’ bora ni Single ya T Pain na 2 Face –’Rainbow’, ‘Khona’ ya Uhuru na Mafikizolo wa Afrika Kusini, ‘Surulere remix’ ya Dk. Sid wa Nigeria, Mkenya Amani ft. Waganda Radio na Weasel ‘Kiboko Changu’ J. Martins ft. Dj Arafat ‘Touching Body’ na Rebees na Wizkid ‘Slow Down’ Tuzo ya msanii bora wa kiume Afrika Mashariki ilikuwa inawaniwa pia na Ben Pol kutoka Tanzania, Bebe Cool wa Uganda, Wyre wa Kenya, Navio wa Uganda na Jackie Gosee wa Ethiopia.
Mtanzania mwingine Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide ameshinda tuzo ya msanii bora wa kike Afrika Mashariki aliyokuwa anashindania na Rema wa Uganda, Aster Aweke wa Ethiopia, Avril wa Kenya, Victoria Kimani wa Kenya na Irene Ntale wa Uganda.
Tuzo ya Mtayarishaji Bora wa video imekwenda kwa Ogopa Dj’s walioitengeneza video ya kwanza ya ‘My Number 1’ ya Diamond Platnumz. Tuzo hizi zilikuwa zinawaniwa na wasanii wa nchi 17

No comments:

Post a Comment

Comments system

Disqus Shortname